| Henry Joseph rasmi Norway |
|
![]() Kiungo mkabaji wa Simba na timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Henry Joseph Shindika, jana alisaini mkataba wa miaka minne kusakata soka ya kulipwa katika klabu ya Kongsvinger ya Norway Kwa mujibu wa wakala wa mchezaji huyo, Mehdi Remtulla, Henry alisaini mkataba kuichezea klabu hiyo inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza nchini humo, ambayo ilianzishwa mwaka 1892. “Kwa sasa timu hiyo ya Kongsvinger inashika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo ya Daraja la Kwanza inayoshirikisha timu 16, ambapo mwishoni mwa msimu, timu mbili zitapanda na kushiriki Ligi Kuu ya Norway,” alisema Remtulla.Kwa mujibu wa Remtulla, Henry amefurahishwa na kufikia makubaliano ya kucheza soka Ulaya, na kuahidi kujituma ili kufungua njia kwa nyota wengine wa Tanzania kufikia hatua hiyo au zaidi. Habari zinasema, chini ya mkataba huo nyota huyo atakuwa akilipwa fungu nono, ikilinganishwa na viwango vya nchini Tanzania, ingawa halikuwekwa bayana.Aidha, Tanzania imepanda kwa nafasi 12 kwa ubora wa soka duniani kwa mujibu wa viwango vya Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), ikitoka nafasi ya 109 hadi 97, huku Brazil ikirejea nafasi ya kwanza kutoka ya tano. Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Florian Kaijage, kwa Afrika, Tanzania sasa inakamata nafasi ya 23, huku ikiwa ya tatu kwa Afrika Mashariki na Kati, nyuma ya Uganda na Sudan.Aidha, Misri ambao ni vinara wa Afrika, wao wanakamata nafasi ya 38 kimataifa, wakifuatiwa na Algeria ambayo kimataifa ni ya 47, huku Tunisia ikiwa ya 49. Akizungumzia mafanikio hayo, Kocha Mkuu wa Stars, Mbrazil Marcio Maximo alisema ni faraja kubwa na kusema hayo ni matokeo ya juhudi ya pamoja wachezaji, benchi la ufundi, TFF , wadhamini na wapenzi kwa ujumla. Maximo alisema, juhudi hizo ndizo zimewafanya wachezaji wa Tanzania waanze kupata soko kimataifa kama kiungo wa Moro United, Nizar Khalfan na Nadir Haroub ‘Cannavaro’.Comments (9)
![]() ![]() written by a guest, July 03, 2009 - 03:28:35
Kazi mzuri kijana, mpira wetu usiishie Bongo tu, laziwe tuwe na impact on international level. Ndugu kacheze boli, tunakutakia kila la heri.
![]() written by a guest, July 04, 2009 - 04:43:27
hongera mazee nenda kawakilishe Tzee majuu, kumbuka huu ni mwanzo tu bado unasafari ndefu kaka, kajitume ili uwafungulie njia na wengine.
big up. Katema, wa Mnarani Beach. ![]() written by a guest, July 05, 2009 - 21:51:55
nenda kacheze mpira hachana majungu hapa nyumbani kwani mafanikio yako ndio yawanasimba pamoja na tanzania kwa jumla mungu ibariki tanzania na ubariki maisha marefu kijana huyu
Baba shani zanzibar ![]() written by a guest, July 08, 2009 - 00:38:36
karibu hapa norway wabongo wenzio tupo wengi hapa tutaksapoti kimtindo kaza boot mwana hiyo ndiyo mofano tunatakiwa kuionyesha dunia kuwa hata wabongo tunaweza. hongera shindika.
![]() written by a guest, July 10, 2009 - 13:58:58
mshikaji nenda ukajitume uwasaidie wanamichezo wengine wa tanzania jitume sana mafanikio ndio yameanza ila ushauri wangu kwako kaka use you tallent to rich the succesfull.Marino from ARUSHA.
![]() written by a guest, July 11, 2009 - 07:48:50
Hongera mwana Henry Joseph Shindika kwa mafanikio yaliyoanza kujitokeza. Watanzania wote tupo nyuma yako. By Kambi Mbwana.
![]() written by a guest, August 07, 2009 - 16:08:12
henry mwana komaa kwani wao wameweza wana nini? huna mpinzani kwenye kiungo.
![]() written by a guest, November 11, 2009 - 07:52:49
safi sana Henry Joseph, nyota nilianza kuiona tangu kwenye umiseta.
Aah mimi kaka yako augustino kalumuna nimeacha mpira si unajua umri tena .Ila kama Maximo angekuja bongo mapema labda ningekuwa Man utd. Big up Write comment
|
Who's been doing what
![]() | ochu othman u want this babe huh come and suck oooh uuuh aaanh shiiit bitch |
![]() | ochu othman added new photos to their profile. |
oh![]() | mh | my ex | my gal | my booo |
| AfriicanAngel updated their profile. |
![]() | kasaka joined our community! Welcome! |
![]() | xaver joined our community! Welcome! |
![]() | nyamundhe joined our community! Welcome! |
![]() | MOGAS joined our community! Welcome! |
The Weather
Dar es Salaam, , TZ
26°C, Windchill: 26°C
Wind: 0 kph N
Humidity: 96%
Visibility: 0 km
Preasure: 1,009 mb steady
Sunrise: 6:28 am
Sunset: 6:38 pm

Hi: 32°C, Low: 27°C

Hi: 33°C, Low: 27°C
Sudoku
|
othman shouts: Gaucho nimekumiza nini kaka?nasikitishwa sana na muafrica wewe kunita mie ni mtu mmbaya sana !!naka |
Latest Songs
| 25688 registered | |
| 6287 female | |
| 19288 male | |
| 20 new this month | |
| New: ochu othman |











