SwahiliEnglish
            Lost Password?    Click here to register

Orodha mpya ya mafisadi yatua Ikulu PDF Print E-mail
Wednesday, 14 May 2008

Orodha ya watumishi wa Serikali wanaotuhumiwa kushiriki katika tukio lililoiwezesha kampuni ya kuzalisha umeme ya Richmond kuingia mkataba wa kifisadi ulioiingiza nchi katika hasara ya mabilioni ya pesa imetua Ikulu kwa ajili ya kusubiri hatua za kiutawala kuchukuliwa dhidi yao.


Akisema na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari, Waziri Mkuu Bwana Mizengo Pinda amesema, mpaka hivi sasa tayari Katibu Mkuu Kiongozi Bw. Philemon Luhanjo ameshakabidhiwa orodha ya wahusika na kupewa maelekezo namna ya kuchukua hatua za kisheria na kiutawala.


Bw. Luhanjo anatakiwa kuchunguza na kuwachukulia hatua watumishi wote wa Serikali wanaotuhumiwa na sakata hilo la mkataba `bomu` wa Richmond, lililozua gumzo kubwa nchini.

Miongoni mwa watuhumiwa waliohusishwa na sakata hilo na kutakiwa kujiuzulu kutokana na kuzembea ama vinginevyo, ripoti ya Kamati hiyo ya Bunge ni pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Johnson Mwanyika, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, TAKUKURU, Bw. Edward Hosea na Mkurugenzi wa Nishati na Madini katika Wizara ya Nishati na Madini Bw. Bashir Mlindoko.


Mapendekezo ya kamati hiyo teule ya Bunge iliyokuwa chini ya Mwenyekiti wake Dk. Harrison Mwakyembe, kigogo mwingine anayepaswa kuchukuliwa hatua za kinidhamu ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Bw. Arthur Mwakapugi.


Kwa mujibu wa Waziri Mkuu Pinda, watuhumiwa hao wanaweza kutimuliwa kazini au kupunguziwa madaraka, kutokana na uzito wa makosa yao au vinginevyo, kadiri sheria zitakavyoruhusu.


``Maelekezo yote amepewa Katibu Mkuu, suala hili sasa linafikia mwisho kwa kuwa anaandaa hatua za kuwachukulia, kama ni kuwafukuza kazi au kuwateremsha vyeo, well and good,``-Bw. Pinda.


Waziri Mkuu amesema hivi sasa Serikali haikubali kuchafuliwa na hivyo kila anayebainika kujihusisha na vitendo vya rushwa na ufisadi anawajibishwa

 

 

Comments
Search
Yassern {space} sijui kweli !!?? Wed, 14th May 08 - 06:09 pm
hatukawii kusikia imechukua mwaka kuwekwa mezani kama vile yaleee majina ya
akina nanihii ya madawa ya kulevya..naona yameshasahaulika, kaazi kweli kweli na
siasa zetu! haya tusikilizie,maana ushikaji kwenye sirikali umezidi
sasa..duh..mungu wee,okoa hii bongo yetu!
Only registered users can write comments!

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Tag it:
Delicious
Furl it!
Spurl
NewsVine
Reddit
YahooMyWeb
Digg
blogmarks
feedmelinks
co.mments
 
< Prev   Next >
Total Members
total 21216 registered
female 5270 female
male 15866 male
month 21 new this month
New: Hapines
Who's Online Now
We have 37 guests online and 13 members online
swejacky Amiry said salehe debra moody x Tito Chamillionaire Danielita Jozeedaking kindgirl Tukwa kelly31 Hapines
Bongo5 Chat Zone 2.0
Total of members in the chatroom:
2006-2007 © Copyright Bongo5.com