SwahiliEnglish
            Lost Password?    Bofya hapa kujiunga





Trafiki akamatwa na `rushwa` ya 3,000/- PDF Print E-mail
Friday, 09 May 2008

Na Hellen Mwango


 

Askari polisi wa kikosi cha Usalama barabarani, maarufu kama trafiki, Sauda Kaijage (39), ameachishwa kazi kutokana na kutuhumiwa kumuomba dereva wa daladala jijini Dar es Salaam, rushwa ya sh. 3,000.

Kutokana na hilo, askari huyo jana aliburuzwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kujibu shtaka hilo.

Aidha, mahakama ilimtaka mshtakiwa huyo kuwa na wadhamini wawili watakaosaini hati ya dhamana ya Sh. 3,000 kila mmoja.

Kaijage alisomewa shtaka lake mbele ya Hakimu Mkazi Benadetha Beda wa mahakama hiyo.

Mwendesha Mashtaka, Inspekta Msaidizi wa Polisi, Francis Mboya, alidai kuwa Machi 31, mwaka huu eneo la Kamata, kati ya Barabara ya Nyerere na Kilwa jijini, mshtakiwa aliomba hongo ya Sh. 3,000 kutoka kwa Samadu Mzallah.

Ilidaiwa kuwa Mzallah ni dereva wa daladala yenye namba za usajili T 781 ALS, na kwamba mshtakiwa aliomba fedha hizo baada ya gari hiyo kuwa na makosa ya kiusalama barabarani.

Mboya alidai kuwa katika shtaka la pili, siku ya tukio la kwanza katika kituo kidogo cha polisi gerezani, mshtakiwa alipokea Sh. 3,000 kutoka kwa Mzallah kwa nia ya kumuachia bila kumlipisha faini kama sheria inavyotaka.
Mshtakiwa alikana shtaka hilo.

Hata hivyo, upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi wa shauri hilo umeshakamilika ambapo mshtakiwa atasomewa maelezo ya awali Mei 22, mwaka huu.

Mshtakiwa alitimiza masharti ya dhamana na yuko nje hadi Mei 22, mwaka huu.

Wakati huohuo, Gloria Michael (31), mkazi wa Sinza jijini Dar es Salaam, amefikishwa mahakamani hapo kujibu shtaka la wizi wa dola 500 za Marekani.

Ilidaiwa kuwa Aprili 22, mwaka huu eneo la Kinondoni jijini, mshtakiwa akiwa kama mtumishi wa ndani, aliiba fedha hizo kutoka kwa muajiri wake, Viviane Abbolt.

Gloria alikana shtaka hilo na kesi itatajwa tena Mei 19, mwaka huu.

 

Source: Nipashe

Tag it:
Delicious
Furl it!
Spurl
NewsVine
Reddit
YahooMyWeb
Digg
blogmarks
feedmelinks
co.mments
Comments
NewSearch
filo - I like the web Fri, 09th May 08 - 12:46 am
To honest and fear i like the web and its people, the web makes us be friends and it helps us discuss issues and arrange events. Bigup :lol: a2YYz
Msambaa - ?? Fri, 09th May 08 - 11:49 am
What has this topic[askari akamatwa na rushwa] to do with web?
GAUCHO Mon, 12th May 08 - 09:24 am
yaleyale bandika ugali mboga naleta sasa hivi! :0 :0
Only registered users can write comments!

 
< Prev   Next >
Total Members
total 19343 wanachama
female 4819 female
male 14442 male
month 661 mwezi huu
Mpya: sweet14
Who's Online Now
We have 36 guests online and 5 members online
melby amachris Iceslim Nisipitwe tamiha
Bongo5 Chat Zone 2.0
Total of members in the chatroom:
2006-2007 © Copyright Bongo5.com