SwahiliEnglish
            Lost Password?    Click here to register





Msimu wa tuzo za Kili wazinduliwa PDF Print E-mail
Wednesday, 07 May 2008
na Dina Zubeiry


KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia ya Kilimanjaro jana ilitangaza kudhamini tuzo za muziki za ‘Kill Music Awards’ kwa mwaka huu, huku kipengele cha fainali ya kusaka washindi wa kanda kikifutwa.

Akizungumza katika hafla ya kutangaza udhamini huo, jana kwenye Ukumbi wa DICC, jijini Dar es Salaam, Meneja wa bia ya Kilimanjaro, Oscar Shelukindo, alisema kwamba, wameondoa fainali za kanda ili kuharakisha kufanyika kwa mashindano ya mwaka huu, kama walivyoelekezwa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).

Alisema, kazi ya upigaji kura kuwachagua wasanii watakaowania tuzo hizo, itaanza Mei 9 hadi Mei 28, kabla ya majaji kuangalia wasanii waliochaguliwa kama wako katika kundi stahili kwa ajili ya kupigiwa kura.

Aliongeza kuwa, uchaguaji huo utatumia njia ya barua pepe, ujumbe mfupi, ‘coupon’ zitakazokuwa kwenye magazeti.

Shelukindo alisema Juni 2, majaji watatangaza majina matano ya wasanii walioteuliwa kuwania tuzo hizo kwa kila kundi, ili wapigiwe kura, zoezi litakalofanyika hadi Juni 4.

Naye Mwakilishi wa BASATA, Angelo Luhala, aliwapongeza wadhamini wa tuzo hizo, kwani zimesaidia kukuza sanaa ya muziki nchini, kwa lengo la kutambua michango ya wanamuziki na washiriki wengine katika tasnia ya muziki.

Vipengele vitakavyowaniwa ni pamoja na mwimbaji bora wa kike, mwimbaji bora wa kiume, albamu bora ya taarabu, wimbo bora wa taarabu, wimbo bora wa Kiswahili (bendi), albamu bora ya Kiswahili (bendi), albamu bora ya R‘n’B, wimbo bora wa R‘n’B, wimbo bora wa asili ya Kitanzania, wimbo bora wa Hip Hop na albamu bora ya Hip Hop.

Nyingine ni wimbo bora wa Reggae/Ragga, albamu bora ya Afrika Mashariki, mtunzi bora wa muziki, mtayarishaji bora wa nyimbo, mtayarishaji bora wa video, mwanamuziki aliyechangia mafanikio makubwa na muda mrefu, wimbo bora wa Zouk na mwanamuziki/ kikundi bora kinachochipukia.

 

Source: Tanzania Daima

Tag it:
Delicious
Furl it!
Spurl
NewsVine
Reddit
YahooMyWeb
Digg
blogmarks
feedmelinks
co.mments
Comments
NewSearch
Only registered users can write comments!

 
< Prev   Next >
Total Members
total 17998 registered
female 4519 female
male 13396 male
month 77 new this month
New: blackbross
Who's Online Now
We have 56 guests online and 9 members online
BAYROS Geoff carine T_pain_Msomali Friiday TANAGWA MIPANGO hegga ferladha
2006-2007 © Copyright Bongo5.com