SwahiliEnglish
            Lost Password?    Click here to register

Mwizi wa kazi za wasanii akamatwa PDF Print E-mail
Friday, 11 April 2008

COSOTA

 

Chama cha Hakimiliki Tanzania (COSOTA) kikishirikiana na jeshi la polisi hivi kaibuni wamemkamata mtuhumiwa mmoja aliykeuwa akijishughulisha na kutengeneza mikanda na CD bandia zenye kazi za wasanii wa muziki hapa nchini.


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Cosota Yustus Mkinga, mtuhumiwa huyo amekamatwa na vifaa vya kutengenezea mikanda na kwamba kazi alizokuwa anadurufu ni jumla ya kazi 90 za wasanii.


Miongoni mwa kazi ambazo zilifumwa zikiwa zimetengenezwa na mtuhumiwa huyo ni pamoja na ya Upendo Nkone, Sikitiko langu, Mizengwe, Lady JD- Moto, Double Extra, Paka Mapepe, Ng?ang?ania, na Msondo.


Nyimbo nyingine ni pamoja na Mapenzi Kizunguzungu, Yebo Yebo, Haleluya Collection, Mtu Pesa, Dar to Lagos, Utalijua jiji na Akudo Impact.
Taarifa hiyo inaeleza kuwa vifaa ambavyo alikuwa akivitumia kufyatulia kazi hizo pamoja na masters za kazi vipo mikononi mwa polisi.


Mkinga amewataka pia wale wote wenye hakimiliki au hakishiriki ya kazi hizo kuwasilisha mikataba na nyaraka nyingine zinazohusu umiliki wa kazi zilizotajwa kabla ya April 12 mwaka huu.


Na hata hivyo mtuhumiwa huyo jina lake halikuweza kupatikana haraka.

 

Comments
Search
Only registered users can write comments!

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Tag it:
Delicious
Furl it!
Spurl
NewsVine
Reddit
YahooMyWeb
Digg
blogmarks
feedmelinks
co.mments
 
< Prev   Next >
Total Members
total 21216 registered
female 5270 female
male 15866 male
month 21 new this month
New: Hapines
Who's Online Now
We have 53 guests online and 17 members online
swejacky QEEN Flojoma debra ara kaga haywire preeety ommy name kanana Chamillionaire nanginyi jeny2 Jozeedaking Tukwa kelly31 Hapines
Bongo5 Chat Zone 2.0
Total of members in the chatroom:
2006-2007 © Copyright Bongo5.com