SwahiliEnglish
            Lost Password?    Click here to register

Mahabusu wazua mgomo gerezani PDF Print E-mail
Wednesday, 09 April 2008

Mahabusu wa Gereza la Keko, jijini Dar es Salaam, jana waligoma kula chakula kwa madai kwamba chakula wanacholishwa ni kibovu kupitilia.


Habari kutoka ndani ya gereza hilo zimedai kuwa mahabusu hao walianza mgomo huo jana asubuhi, kwa madai kwamba wamechoshwa kulishwa dona.


“Ni kweli kabisa mahabusu wa Gereza la Keko wamegoma kula chakula kuanzia asubuhi, kwa madai kwamba chakula wanacholishwa hakifai kwa matumizi na afya ya binadamu.


“hapo mwanzo walikuwa wakilishwa sembe lakini ghafla hivi karibuni wameanza kulishwa dona na kwa kweli wana haki ya kugoma kula chakula hicho, kwa kuwa ni kibaya na hakina ladha mdomoni,” alisema mtu mmoja aliyezungumza na mtandao huu jina limehifadhiwa.


Vyanzo kutoka ndani ya gereza hilo, vilibainisha kuwa, mahabusu hao wameapa kuendelea na mgomo wao wa kutokula chakula hicho, hadi uongozi wa gereza hilo utakapowabadilishia mlo wao.


Habari kutoka gerezani humo zilieleza kuwa, mahabusu hao walifanya mgomo huo wakiwa katika hali ya utulivu uliokithiri bila kelele wala fujo, tofauti na ilivyozoeleka hasa wanapokuwa katika kipindi cha mgomo.


Mwaka jana mahabusu kutoka magereza mbalimbali hapa nchini wakiwemo wa Keko, waligoma kushuka kwenye makarandika kwa ajili ya kuudhuria kesi zao katika mahakama mbalimbali nchini, kwa madai kadhaa.


Mahabusu hao walikuwa wakilalamikia kucheleweshwa kwa kesi zao na mlundikano wa mahabusu katika magereza.

Comments
Search
Only registered users can write comments!

3.26 Copyright (C) 2008 Compojoom.com / Copyright (C) 2007 Alain Georgette / Copyright (C) 2006 Frantisek Hliva. All rights reserved."

Tag it:
Delicious
Furl it!
Spurl
NewsVine
Reddit
YahooMyWeb
Digg
blogmarks
feedmelinks
co.mments
 
< Prev   Next >
Total Members
total 21216 registered
female 5270 female
male 15866 male
month 21 new this month
New: Hapines
Who's Online Now
We have 51 guests online and 18 members online
swejacky Amiry QEEN Flojoma debra ara kaga haywire preeety ommy name kanana Chamillionaire nanginyi jeny2 Jozeedaking Tukwa kelly31 Hapines
Bongo5 Chat Zone 2.0
Total of members in the chatroom:
2006-2007 © Copyright Bongo5.com