|
Thursday, 07 January 2010 |

Mvutano unaoendelea kati ya Shirika la umeme nchini (TANESCO) na kanisa la Gospel Bible Fellowship Church (GBFC) linaloongozwa na Kakobe unaendelea kushika kasi hata baada ya msemaji wa shirika hilo kusema kwamba upitishaji wa umeme kwenye kanisa hilo hautaathiri usalama wa waumini. Waumini hao wanakesha kanisani hapo usiku na mchana wakiimba nyimbo za kuliusia Shirika hilo kumwogopa Mungu
|
|
Thursday, 07 January 2010 |

Mchezaji wa mpira wa kikapu kwenye ligi ya NBA, Shaquille O'Neal amekumbwa na skendo ya kulazimisha mapenzi kwa msichana mmoja anayefahamika kwa jina la Vanessa Lopez. Hata hivyo, polisi wamebaini kuwa msichana huyo ameshawahi kujipendekeza kwa wachezaji Kenyon Martins wa Denver Nuggets na Delonte West wa Cleveland Cavaliers na hivyo kupunguza uzito wa madai yake. Shaq bado hajatoa tamko lolote kuhusiana na sakata hilo
|
|
Rais ala msosi na wachezaji |
|
Thursday, 07 January 2010 |
|

Wachezaji wa timu za taifa za Ivory Coast, Rwanda na Tanzania jana walipata wasaa wa kula lanchi na Rais Jakaya Kikwete kwenye hoteli ya Golden Tulip. Akitoa shukrani, Rais aliwashukuru wachezaji wa Ivory Coast kwa ziara yao na kuwatakia mafanikio kwenye michuano ya soka Afrika huko Angola. Wageni watacheza na Rwanda leo na kuondoka kesho kuelekea Angola kwenye kipute hicho
|
|
Elizabeth ndani ya Filamu |
|
Wednesday, 06 January 2010 |
|

Aliyekuwa mshiriki katika shindano la Big Brother Africa Revolution kutoka Tanzania, Elizabeth Gupta, ameshiriki katika filamu mpya kabisa ya 'Danger Zone: Himaya ya Hatari' iliyotengenezwa na Kampuni ya RJ Company. Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Vincent Kigosi amesifu kipaji kilichooneshwa na Elizabeth na kukubali kweli mtoto anaweza. Milango inazidi kufunguka kwa Elizabeth na kumpatia michongo kibao. Mungu awe naye
|
|
Wednesday, 06 January 2010 |
|

Bado kidogo hali ya hewa ichafuke huko Las Vegas wikiendi iliyopita baada ya kambi ya Bondia Floyd Mayweather Jr kuvimbishiana vifua na ile ya Rapa Rick Ross kwenye pati kufungua ukumbi wa Disko wa Vanity iliyoandaliwa na Diddy kwenye mgahawa wa Hard Rock Cafe
|
|
BB UK kupanda Kilimanjaro |
|
Wednesday, 06 January 2010 |
|

Waliowahi kuwa washiriki wa Big Brother celebrity UK, Liam Mc Gough na Anthony Hutton pamoja na rafiki yao Zach Lichman na mapacha Amanda na Samantha Marchant, watakuwa nchini kuanzia Juni 18 kupanda Mlima Kilimanjaro kwa hisani ya MAD ( Make A Difference) Foundation ili kuchangia fedha za kusaidia jamii
|
|
<< Mwanzo < Prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 Next > Mwisho >>
|