|
Monday, 11 January 2010 |

Nani mrefu kati ya galacha wa hip hop nchini Anselm Ngaiza aka 'Soggy Doggy Anter' na staa wa Orijino Komedi Lucas Mhuvile aka 'Joti'?
|
|
Monday, 11 January 2010 |

Mwanamuziki na mdau mkubwa wa mzuki wa hip hop, Saigon, ameachia ngoma
ya kufungua mwaka inayokwenda kwa jina la 'Soma' iliyotengenezwa kwenye
studio za Tongwe Records na prodyuza J Ryder. Kwa mujibu wa Saigon,
ametoa ngoma hiyo kuwahamasisha watanzania, hasa vijana kujijengea
utaratibu wa kusoma ili kuondokana na ujinga. Huo ni mwanzo tu kwa Saigon kwani kwa sasa yuko kwenye harakati ya kutoa albamu yake atakayoifanya kwenye studio tofauti
|
|
Monday, 11 January 2010 |

Habari za kusikitisha zilizofika dawatini ni kuporwa kwa mkoba wa mwanamuziki Lady JD. Tukio hilo la kusikitisha lilitokea usiku kwenye uwanja wa taifa wakati timu ya soka ya taifa ilipomenyana na Ivory Coast kwenye mechi ya kirafiki. Ishu ilikuwa wakati akitoka akiwa na marafiki zake, miongoni akiwepo mlinda mlango maarufu wa Simba, Juma Kaseja ambapo inadaiwa kundi la vibaka wakiwa na bisibisi na mapanga liliwavamia wakati wakielekea kwenye maegesho ya magari na kupora mkoba huo. Haijafahamika bado thamani ya vitu vilivyokuwemo ndani 'kipima joto' hicho
|
|
Monday, 11 January 2010 |
|

Rihanna ameonekana na mpenzi mpya wakati wa sikukuu ya mwaka mpya Dubai na Mexico. Jamaa anaitwa Matt Kemp na anacheza mpira wa magongo Marekani akiwa na timu ya L.A Dodgers. Picha zinawaonyesha wakiwa kwenye mahaba mazito. Chris Brown alitumia mikono kumtwanga Rihanna kwa sababu ndiyo anatumia zaidi akiwa stejini, sasa jamaa anatumia magongo uwanjani. Sijui itakuwaje ikitokea mikorogano
|
|
Monday, 11 January 2010 |

Kufuatia shambulio lililopelekea kupoteza maisha ya wachezaji 2, dereve wa basi, kocha msaidizi na afisa habari huko mjini Cibanda, timu ya taifa ya Togo haitashiriki kwenye michuano ya kombe la mataifa ya Afrika pamoja na kuimarishwa ulinzi. Rais Faure Gnassingbe alituma ndege ya Rais kuwachukua wachezaji hao ambao awali walikubaliana kucheza kwenye michuano hiyo kwa heshima ya wenzao waliofariki. Washabiki wa mpira watakosa manjonjo ya Adebayo waliyokuwa wakitegemea kuyapata
|
|
Monday, 11 January 2010 |

Wenyeji wa michuano ya soka kwa mataifa ya Afrika, Angola, jana walishindwa kuamini macho yao kwenye ufunguzi wa michuano hiyo baada ya Mali kurudisha magoli 4 ndani ya dakika 11 za mwisho za mchezo huo. Mpaka dakika ya 79, Angola walikuwa mbele kwa magoli 4-0. Juhudi zilizofanywa na wachezaji wa Mali wakiongozwa na mshambuliaji wao anayechezea Sevilla, Steven kanoute zilizaa matunda baada kuongeza mashambulizi na kufanikiwa kurudisha magoli yote 4 na kuufanye mchezo huo uishe kwa sare
|
|
<< Mwanzo < Prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 Next > Mwisho >>
|