|
Cowell aitosa American idol |
|
Wednesday, 13 January 2010 |
|

Mmoja wa majaji aliyeleta mafanikio kwenye mashindano ya kusaka vipaji ya American idol, simon cowell, ataondoka na kujiunga na mashindano aliyoanzisha mwenyewe ya X factor nchini Uingereza. Msimu huu utakuwa wa mwisho kwa Cowell ambaye inasemekana anabadilisha mazingira kusaka maslahi zaidi ingawa awali alikuwa anatengeneza zaidi ya Dola milioni 36 kwa mwaka
American Idol ndiyo iliyowatoa wasanii kama Rubben studdard, Fantasia na Kelly Clarkson
|
|
Ali Kiba ndani ya reading, UK |
|
Wednesday, 13 January 2010 |

Mpango mzima unasababishwa na Bongo DJs na utakuwa siku ya Januari 30 huko kwa Malkia Elizabeth
|
|
Mrema asafishwa na wenzie |
|
Wednesday, 13 January 2010 |
|

Naibu katibu mkuu wa TLP, Hamad Rajab Tao leo amezindua kitabu kinachoelezea undani wa mvurugano unaoendelea katika chama hicho kwenye mkutano na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa habari maelezo. Kwenye kitabu hicho, katibu ameelezea kashfa zinazomuandama Mwenyekiti wa taifa wa TLP. Ndg Augustine Mrema na kusema kwamba hazina ukweli wowote. Miongoni mwa kashfa hizo ni kubinafsisha nyumba ya chama na kutumia shilingi milioni 15 kununua nyani wa Kampeni
|
|
Tuesday, 12 January 2010 |

Mahakama ya Hakimu mkazi ya Kisutu imetoa haki ya kukamatwa kwa mwanasiasa mkongwe nchini, Mch. christopher Mtikila baada ya kushindwa kufika mahakamani katika muda uliopangwa kusikilizwa kesi dhidi yake ya kumkashifu Rais Jakaya Kikwete kwa kumwita gaidi, kosa analodaiwa kutenda Oktoba 21 mwaka jana kwenye maghorofa ya NHC Ilala. hata hivyo baadaye alifika mahakamani hapo na kukumbana na mkono wa sheria
|
|
Tuesday, 12 January 2010 |
|

Kocha muingereza Stewart Hall ameielezea nia yake ya kurithi mikoba ya Mbrazil Marcio Maximo kuinoa Taifa Stars. Hall, ambaye ameshawahi kuzifundisha timu za taifa za Trinidad & Tobago na St. Vincent & Grenades na klabu ya India ya Pune FC, amesema hivyo kupitia Uk Press huko ikiwa imebaki miezi michache mkataba wa Maximo kumalizika na amesisitiza umuhimu wa kuwanoa makocha wazalendo ili kuinua soka nchini
|
|
Dully anakuja na 'Tapatapa' |
|
Tuesday, 12 January 2010 |

Kama ulifikiri ngoma ya Shikide kutoka kwa Dully Sykes ndiyo ngoma kali kuliko zote za Dully, fikiri tena. Jamaa ameing'ata Bongo5 sikio kuwa mwezi Machi ataachia ngoma mpya kwa mwaka huu 'Tapatapa' au Top of the toppest ambayo imekaa kibata kupita maelezo. Audio zimefanyika kwenye studio za Dhahabu recordz na kwa sasa yuko kwenye harakati za kutengeneza video na Visual lab
|
|
<< Mwanzo < Prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 Next > Mwisho >>
|