|
Friday, 15 January 2010 |
|
Taasisi ya taaluma za kiswahili Chuo kikuu cha Dar es salaam kinakuletea tamasha kubwa la Bongo Fleva linaloitwa Elimika na Bongo Fleva ikwa ni mchango wao katika kukuza muziki wa kizazi kipya. Ukiachana na burudani zitakazotoka kwa wasanii kama Afande Sele, Zay B, THT na wengine wengi, kutakuwa na maonyesho ya kazi za wasanii kama fulana, graffiti n.k kwenye mabanda yatakayowekwa maalum kwa shughuli hiyo. Pia kutazungumzwa mada mbalimbali, mgeni rasmi akiwa Prof. HJM Mwansoko wa Wizara ya Habari na utamaduni. Ishu nzima ni Jumamosi na Jumapili ijayo, kiingilio Bure
|
|
Friday, 15 January 2010 |

Mtayarishaji wa Filamu anayefanya vizuri na kampuni yake ya Chapakazi Films, Adili Hisabati, anauanza mwaka vyema kwa kuachia filamu inayokwenda kwa jina la Loleza ikiwa imesheheni vichwa kama Buff G, Mansu Li, Adili mwenyewe na mdogo wake Ibrahimu. Adili anasema si filamu ya kuikosa na itakuwa mitaani kuanzia mwezi wa pili
|
|
Friday, 15 January 2010 |

The premier himself, Hon. Mizengo Pinda, has come forward and declared his property publicly. Speaking with the press yesterday, the PM said he owns only two houses one in Dodoma and the other in Mpanda, his homeland, and an unfinished house at Pugu. His bank account balance, he claims, does not exceed Tshs 25 milion
|
|
Lupe Fiasco ndani ya Bongo |
|
Thursday, 14 January 2010 |

Msanii wa Marekani, Lupe Fiasco, yupo nchini tangu Januari 11 akipanda mlima Kilimanjaro kwa hisani kwenye kampeni ya kusisistiza matumizi ya maji safi katika nchin zinazoendelea. Miongoni mwa watu maarufu walioambatana na msanii huyo, ni mwigizaji wa Marekani Jessica Biel na mwanamuziki Kenna mwenye asili ya Ethiopia. Upandaji wa mlima huo utachukua siku saba na baada ya hapo jamaa atarudi kwao kuendele kula bata. Shughuli hiyo imedhaminiwa na kituo cha burudani cha MTV
|
|
Thursday, 14 January 2010 |
|

Mchezaji wa Serbia ambaye pia anachezea klabu ya Manchester United, Nemanja Vidic, anaamini timu ya Serbiaitafanya vizuri kwenye fainali za kombe la Dunia baadaye mwakani huko Afrika Kusini na kufanikiwa kupita hatua za awali. Vidic anasema Serbia imejiandaa vizuri ikiwa na wachezaji bora kushinda zadi ya awali walipocheza huko Ujerumani Hii ni mara ya kwanza kwa mchezaji huyo kucheza kwenye fainali hizo ingawa alikuwepo kwenye benchi kwenye fainali za mwaka 2006 zilizofanyika Ujerumani
|
|
Thursday, 14 January 2010 |
|

Waumini wa kanisa la Full Gospel Bible Fellowship bado wanaendelea kupiga kambi usiku na mchana kwenye kanisa lao maeneo ya Sinza kwa kupokezana zamu kupinga hatua ya TANESCO kupitisha umeme kwenye kanisa hilo

Hata hivyo, waumini hao waligoma kuongea na mwandishi wa Bongo5 na kusema msemaji wa swala hilo ni Askofu Kakobe peke yake
|
|
<< Mwanzo < Prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 Next > Mwisho >>
|