|
Wyclef alivyoguswa na Haiti |
|
Tuesday, 19 January 2010 |

Mwanamuziki na prodyuza wa Marekani ambaye asili yake in Haiti, Wyclef jean, kupitia Taasisi yake ya Yelle haiti akishirikiana na AmeriCares na friends of WFP, amefanikiwa kuchangisha zaidi ya Dola milioni 2 kusaidia wahanga wa tetemeko la ardhi lililotokea wiki iliyopita huko Haiti na kuwaacha maelfu bila makazi. Clef aliweka ujumbe kwenye wavuti ya taasisi hiyo akiwaomba watu wajitolee kusaidia waathirika na kupata kiasi hicho cha pesa
|
|
Tuesday, 19 January 2010 |

Taasisi isiyo ya kiserikali wala kibiashara ya Peercorps Trust Fund, imezindua jamii salama yenye malengo ya kupunguza maambukizi ya VVU, kuboresha maisha ya kijijini hasa kwa mama na mtoto, kuboresha elimu na usawa na pia kuzuia ajali. Akiongea na waandishi wa habari leo kwenye ukumbi wa maelezo, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, Dr. Hamis Kigwangalla, amefafanua kwamba nchi nyingi zinazoendelea zimekuwa na wakati mgumu kupambana na ajali kutokana na kuwa na uwezo mdogo kiuchumi hivyo kupoteza nguvu kazi za nchi na kuzidisha umaskini, sababu iliyowapelekea kuzindua Jamii hiyo wakishirikiana na Taasisi ya Kiswidishi ya Karolinska
|
|
Monday, 18 January 2010 |
|

Mjengo wake

Usafiri wake
Zay B aka Mwanadada gaidi ameibuka na kusema kuwa kimya chake kingi hakimaanishi kwamba amefulia kimuziki ila ni kutokana michongo inayomuingizia hela zaidi ya muziki wa bongo ambao bado haulipi. Mdada kwa sasa anamiliki Toyota Premio na yuko kwenye harakati za kumalizia mjengo wake pande za Buyuni, Pugu. Kama hiyo haitoshi, Zay B anasema kwa sasa yuko kwenye mkataba wa kufanya kazi za muziki na kampuni ya Butile Africa Group ya Afrika Kusini. Kuna lingine?
|
|
Monday, 18 January 2010 |
|

Mgosi....Mwiba wa Majimaji
Jerry Tegete na Mrisho Ngassa walifunga magoli katika dakika ya 23 na 75, na kuwainua mashabiki wa Yanga siku ya Jumamosi pale timu hiyo ilipoilaza African Lyon Jumamosi na kufikisha pointi 24 nyuma ya Simba ambao nao walishuka dimbani na kukausha Majimaji ya Songea kupitia kwa Mussa Hassan Mgosi dakika ya 39 na 72 mabao 2 kwa bila. Spidi ya Simba bado iko kwenye mshale wa 120 ikiwa na pointi 36 baada ya kushinda mechi 12 katika la ligi
|
|
Monday, 18 January 2010 |

Prodyuza 'yanki' anayepiga dili kupitia game ya muziki wa kizazi kipya, Victor Faiz Bahaj ameamua kuingiza voko mwenyewe huku akimpa shavu staa wa sanaa hiyo, Rehema Chalamila a.ka. Ray C.
|
|
Monday, 18 January 2010 |

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Nuru Mohd aka Nuru the Light, anatarajia kufanya show kambambe pale Florida KeyWest, Oyster Bay maeneo ya kilimanyege siku ya Jumatano
tarehe 20 Januari.
|
|
<< Mwanzo < Prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 Next > Mwisho >>
|