|
Well, kama nimeelewa vizuri, wanazungumzia vitambulisho vya ukaazi, na sio vitambulisho kwa ajili ya kuingia z'bar.
Tatizo ambalo linaliona hapo ni kwa masheha kugeuka miungu watu, kwani wao ndio wanaopaswa kutoa idhini ya mtu yoyote kupata kitambulisho cha ukaazi...
Kabla ya kuanza kwa zoezi hili, iliwahi kuripotiwa kuwa ili uweze kuwa mkaazi wa z'bar, inakupasa kuishi ndani ya visiwa hivyo kwa muda wa miaka mitano mfululizo....
Kwa wale ambao hawana nia ya kuwa wakaazi wa visiwa hivyo sidhani kama sheria hii inawahusu, zAidi labda watapata usumbufu mkubwa kutoka kwa polisi, JKU , KMKM, na kikosi cha voluntia, kwani ile habari ya kutembea na kipande kama Kenya ndio sasa inabisha hodi Visiwani humo...!
|