SwahiliEnglish
            Lost Password?    Click here to register




 

Results 271 - 300 of 2005
Anayejulikana kama Meneja wa kundi la Wanaume Halisi bwana King Kiboya kwa jazba kubwa sana baada ya kuona vijana wake wanakamua ile mbaya alibahatika kukutana na mwandishi wa Mtandao huu na kumtaka aweke wazi kwa wasomaji...

Wiki iliyopita tuliandika juu ya ujio wa wasanii maarufu duniani wa kundi la G-Unit nchini Afrika Kusini ambapo zilizuka hoja nyingi zilizokuwa zimedai kuwa ujio huo kwa Tanzania bado ni ndoto...  

Baadhi ya Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, wamehoji sababu za Mbunge wa Igunga, Bw. Rostam Aziz, kutopewa fursa ya kujieleza kuhusiana na tuhuma zinazomkabili kwa mujibu wa Kamati Teule ya Bunge

Spika wa Bunge, Bwana Samuel Sitta amewaacha hoi waheshimiwa wabunge alipotoa taarifa ya utafiti kuhusu wanaume wanaopigwa na wake zao huko majumbani kwao

"Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imetakiwa kuwachukulia hatua kali za kisheria watuhumiwa wa ufisadi wa mabilioni ya shilingi katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA)"- Tundu Lissu

Chama cha Hakimiliki Tanzania (COSOTA) kikishirikiana na jeshi la polisi hivi kaibuni wamemkamata mtuhumiwa mmoja aliykeuwa akijishughulisha na kutengeneza mikanda na CD bandia zenye kazi za wasanii wa muziki hapa nchini

Wakati watu 172 wanaotuhumiwa kuhusika na mauaji kutokana na imani za kishirikina, hususani albino, wakiwemo waganga wa jadi 71 wametiwa mbaroni

MSEMAJI wa Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Rwanda (ICTR), Roland Amoussouga jana aliwahuzunisha waandishi wa habari baada ya kuelezea alivyoshuhudia maiti za watu waliouawa nchini Rwanda wakati wa mauaji ya kimbari

Kama itakumbukwa mnamo tarehe 2/4 wanafamilia wa bongo5 walipoteza moja wa wanachama wao aliyefariki huko Leeds nchini Uingereza, taratibu za kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka uingereza zimefanyika kwa ushirikiano wa ndugu na jamaa wa marehemu

Yule mshindi wa wa pili wa shindano la Big Brother Afrika 2,Tatiana Durao wa Angola anatarajia kushuka nchini Aprili 22 katika ziara fupi itakayoambatana na maonesho mbalimbali ya mavazi na urembo

Ni mwezi mmoja tangu Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Mbeya kuwaachia huru watuhumiwa 11 wa usafirishaji wa dawa za kulevya kupitia tumbo la marehemu Kombo Siriri, Jeshi la Polisi Mbeya limekamata aina mpya ya dawa hizo

Balozi Maluum wa Marekani (Uhalifu wa Kivita), Clint Williamson ameahidi na kusisitiza kuwa ile kutoa tuzo ya dola milioni 5 za Marekani (sawa na zaidi ya Sh 5 bilioni za Tanzania) iko pale pale kwa watakaotoa taarifa

MAREKANI na Uingereza, zimewaonya Rais Mwai Kibaki na Waziri Mkuu Mtarajiwa Raila Odinga na kuwataka kumaliza tofauti zao kwa haraka na kutangaza Baraza la Mawaziri.

Michuano ya kumtafuta Pop Idol ambayo inawahusisha washiriki wanne kati ya 1000 waliojitokeza kuwania tiketi ya kwenda jiji Nairobi kwa ajili ya kuiwakilisha Tanzania, wamefanikiwa kupata nafasi hiyo na mpaka sasa wako katika maandalizi

Unaweza kusema hii ni kali kati ya kali ambazo zimewahi kujiytokeza ulimwenguni, ambapo mwanaume aliyepata ujauzito hivi karibuni ameamua kujiweka hadharani kwa kuitangazia dunia kuhusiana na jinsi ameizoea hali yake hiyo

Mahabusu wa Gereza la Keko, jijini Dar es Salaam, jana waligoma kula chakula kwa madai kwamba chakula wanacholishwa ni kibovu kupitilia

Kampuni ya Richmond Development ambayo ilipewa dhamana ya kuagiza mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura na shirika la umeme Tanesco hivi karibuni imesema hawahusiki na haikuwahi kupokea fedha yoyote kutoka serikalini

Kijana mmoja muuza magazeti amekufa papo hapo baada ya kufunikwa na magari zaidi ya matatu kati ya nane yaliyopata ajali baada ya Fuso kukatika breki, tukio hilo lilitokea jana jijini Dar es Salaam maeneo ya Ubungo

JINAMIZI la tuhuma za ufisadi zilizosambazwa katika mtandao wa intaneti zikimlenga Spika wa Bunge, Samuel Sitta, sasa zinaonekana kuvuka mpaka na kuanza kuigusa na kuisumbua familia yake

KUNDI la majambazi wenye bunduki mbili aina ya SMG, mashoka, mapanga na marungu, wameteka kijiji cha Kangeme kata ya Ulowa wilayani Kahama na kupora maduka zaidi ya 20 huku wakiimba nyimbo za kumsifu Rais George Bush

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-moon tarehe 7 alitoa taarifa ikieleza kufuatilia kutotangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa urais baada ya uchaguzi wa urais wa Zimbabwe kufanyika siku 9 zilizopita

Mkurugenzi wa bendi ya TOT, maarufu sasa kama T-Respect, Kapteni mstaafu John Komba, amesema kwamba wamefanya mapinduzi ya hali ya juu, hivyo wapinzani wao wakae chonjo kwani wanakuja na ‘spidi’ kali

CHAMA cha Wananchi (CUF) kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kutekeleza moja kati ya mambo mawili, kama masharti ya kutaka kurejesha imani ya chama hicho kwake

SERIKALI imeingilia kati na kumaliza mgogoro kati ya wafanyakazi na wawekezaji wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) kwa kuamua kubeba mzigo wa kulipa mishahara ya miezi mitano ambayo itagharimu sh. bilioni 3.6

MELI isiyofahamika iliyokuwa na abiria na wafanyakazi 14, imezama katika Bahari ya Hindi mwishoni mwa wiki.

Wanandoa wameuawa kikatili kwa kupigwa mawe na kuchapwa viboko hadi kufa huku wakiwa wamefungwa kamba na wananchi wilayani Karagwe mkoani Kagera

CHAMA cha Wamiliki wa Magari ya Abiria Mkoa wa Dar es Salaam (DARCOBOA), kimesema kinakamilisha taratibu za kuwatoza nauli askari wa majeshi yote nchini na kuongeza nauli ya wanafunzi kufikia Sh 100

Inasemekana msanii Nyota wa muziki Rihanna kuwa ana mahusiano ya kimapenzi na msanii Chris Brown, jambo ambalo wote kwa pamoja wamekuwa wakilikanusha vikali huku wakidai wao ni marafiki tu

Jumuiya Ya Watanzania Uingereza inasikitika kutangaza kifo cha mwanajumuiya wa Kitanzania Bi. Mwajuma Ibrahim Seif, kilichotokea jana katika hospitali ya Royal Berkshire Hospital, Reading

MUASISI wa hoja ya kuurejesha muafaka wa kisiasa visiwani kwa wananchi, kwa njia ya kupigwa kura ya maoni, ni Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Amani Abeid Karume, imefahamika

  

Powered by AlphaContent Bongo5.com © 2005-2008 - All rights reserved
Total Members
total 19348 registered
female 4821 female
male 14445 male
month 666 new this month
New: KITOJO
Who's Online Now
We have 36 guests online and 11 members online
Marc my rachel halfa k nyaksy BUDDY Rashid10 sifa Elmi faddymbongo Thabit tudes
Bongo5 Chat Zone 2.0
Total of members in the chatroom:
2006-2007 © Copyright Bongo5.com