Burudani
Collabo kati ya Fid Q na rapper wa Ghana, Sarkodie yanukia
Rapper Fareed Kubanda aka Fid Q atamshirikisha rapper wa Ghana, Sarkodie kwenye ngoma yake mpya.
Diamond ndiye aliyemuunganisha Fid na rapper huyo anayeheshimika barani Afrika na miongoni mwa wasanii matajiri zaidi.
Akiongea kwenye kipindi cha Genge cha EFM leo, Diamond alidai alimuunganisha Fid na staa huyo baada ya kumsikia kuwa angependa kufanya naye na hivyo kumtumia ujumbe kumwambia kuwa ‘rapper namba moja’ Tanzania angependa kufanya naye wimbo.
Alidai kuwa alimtumia clip fupi ya Fid akitumbuiza na Sarkodie kushangaa jinsi Ngosha alivyokuwa akishangaliwa pamoja na uwezo wake. Tayari Sarkodie ameshatumiwa wimbo atakaoshirikishwa na Ngosha.