Burudani
Christian Bella aeleza kwanini mara nyingi husikiliza nyimbo za Chris Brown, Justin Bieber na wasanii wengine wa Marekani
Muimbaji wa muziki wa dansi na hitmaker wa nyimbo kama ‘Usilie’ na ‘Msaliti’ Christian Bella amesema mara nyingi husikiliza nyimbo za wasanii wa Marekani hasa wa muziki wa R&B na Hip Hop kwakuwa humpa uwezo wa kubadilika katika utunzi wa nyimbo zake.
“Namsikiliza sana Chris Brown, nasikiliza sana nyimbo za kizungu, nasikiliza akina Justin Bieber. Nasikiliza hata wasanii wanaochana kama akina Soldier Boy, mimi ndo vitu vyangu hivyo,” amesema Christian. “Nasikiliza mavitu international sana, inanipa mimi akili huwezi kuamini. Mimi pia najifunza jinsi gani wao wanacheza na sauti, wao wanakaa vipi kwenye gitaa, ofcourse inaniongeza mimi akili fulani ambayo mtu hawezi kuelewa,” ameongeza.