Burudani
Chidi Benz apata dhamana baada ya kutimiza masharti
Rapper Rashid Makwiro aka Chidi Benz amepata dhamana baada ya kutimiza masharti ya kesi yake ya kukamatwa na dawa za kulevya.
Jana Chidi alipandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na kusomewa mashtaka matatu ya kukutwa na madawa ya kulevya ambapo alishindwa kutimiza masharti ya dhamana ya shilingi milioni 1 pamoja na wadhamini wawili wasiokuwa na hatia.
Kesi yake itasikilizwa tena Novemba 11 mwaka huu.
Source:EATV/Globalpublishers