Burudani
Chibwa amuongeza Hard Mad kwenye wimbo ujao
Mkali wa muziki wa Dancehall Bongo, Chibwa amesema wimbo aliofanya na Hard Mad ndiyo unaofuata.
Hivi karibuni Chibwa aliachia wimbo wake mpya aliomshirikisha msanii kutoka Jamaica, Elephant Man na kuahidi kuachia video ya wimbo huo baada ya miezi miwili au mitatu.
Akizungumza na Bongo5, Chibwa amesema ‘wimbo wangu unaofuata nitauachia niliofanya na Hard Mad’.
“Nimefanya kazi nyingi za kimataifa, lakini kazi inayopewa nafasi kubwa na uongozi wangu ni wimbo niliofanya na Hard Mad. Baada ya kuachia video ya wimbo wa Dancehall Digital nitaachia wimbo niliofanya na Hard Mad,” aliongeza.