Burudani

Chibu Perfume ya Diamond kuingia sokoni muda wowote

Chibu Perfume za mkali wa wimbo Salome, Diamond Platnumz zitaingia sokoni muda wowote kuanzia sasa kwa mujibu wa Sallam, meneja wa masanii huyo.

Mwaka 2016 muimbaji huyo alionyesha sample ya perfume hizo hali ambayo ilileta shauku kumbwa kwa mshabiki wa muimbaji huyo.

Ijumaa hii meneja wa msanii huyo, kupitia ‘Insta Live’ amedai tayari mzigo wa perfume hizo umeshaingia mjini na utapatikana katika maduka mbalimbali nchini.

“Mzingo umeingia, utapatikana kila sehemu bado hatujapanga bei,” alisema Sallam huku akionyesha perfume hizo.

Meneja huyo alidai perfume hizo hazitapatikana kwa bei ya chini ya laki moja na huwenda bei ikaongezeka kutokana na ubora manukato hayo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents