Michezo

Chelsea yapeta bila Diego Costa

Vinara wa ligi kuu ya England, Chelsea waliendelea kujikita kileleni kwa kuwachakaza mabingwa watetezi Leicester City kwa mabao 3-0 bila ya mshambuliaji wake tegemezi ambaye inasemekana ana matatizo Na benchi la ufundi, Diego Costa.

Chelsea walipata mabao yao kupitia Marco Alonso aliyeingia kambani mara mbili, huku mshambuliaji wa kihispania Pedro akimalizia msumari wa mwisho kwa kupachika bao la tatu.

Matokeo ya mechi za awali Spurs na Arsenal walipaata ushindi wa goli 4 kila mmoja. Spurs walichakaza Westbromwich kwa mabao ya Harry Kane aliyefunga mara tatu ‘hat-trick’ na goli la kujifunga la G McCauley. Magoli ya Arsenal yalifungwa na Olivier Giroud, Alexis Sanchez na magoli mengine ya kujifunga ya J. Cork na K Naughton.

Kwingineko nchini Hispania Lionel Messi Na Suarez waliongoza mauaji dhidi ya Las Palmas kwa ushindi wa mabao 5-0, Suarez – 2, Messi – 1, A.Turan – 1 na A.Vidal – 1.

Matokeo mengine: Burnley 1-Soton 0 , Hull City 3-B’mouth 1, Westham 3-C.Palace 0, Watford 0- M’boro 0,Sunderland 1- Stoke 3.

By Eliezer Gibson greencitynative

IG:gibson_elly

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents