Burudani
Chege na Temba kurudi studio kuandaa wimbo wao mpya
Wasanii wa muziki kutoka TMK Family, Chege na Temba leo wanaingia studio ya Mkubwa na Wanae kuandaa wimbo wao mpya wa mwaka huu.
Akizungumza na Bongo5 leo, Chege amesema wanaanza kurekodu leo wimbo huo utakaotoka mwezi ujao.
“Leo tunaanza kurekodi wimbo wetu mpya katika studio ya ‘Mkubwa na Wanae’,” amesema. “Wimbo utatoka mwezi wa tatu,kwahiyo mwaka huu tumejipanga muziki wetu uwe wa kibiashara zaidi ndani ya nchi na nje. Tutakuwa hatuna wasiwasi,uhakika. Ndio maana uongozi wa TMK Family ukasuggest mwaka huu Chege na Temba laziwa wafanye kazi ya pamoja.”
Wimbo wa mwisho wa Chege na Temba uliotoka ni ‘Tunafurahi’.