Burudani
Chege ‘kuchapa hit nyingine’ kwa kuachia wimbo mpya ‘Wauwe’
Msanii wa kundi la Wanaume Family, Chege Chigunda amesema ingawa wimbo wa ‘Chapa Nyingine’ unaendelea kufanya vizuri, anatarajia kuachia wimbo mpya ‘Wauwe’ ambao upo tayari.
Akizungumza kwenye kipindi cha The Playlist cha Times FM jana,Chege amesema wimbo huo ulitayarishwa mwezi uliopita.
“Kimuziki formation ni ileile Chapa Nyingine ,sisi tunatoa ngoma tu ,tunatoa ngoma baada ya ngoma,kwahiyo this time kuna mambo yameandaliwa soon itaachiwa. Kuna wimbo tayari tumeshaufanya unaitwa ‘Wauwe’ kwahiyo watu wakae mkao wa kula tu,” alisema.