Burudani
Chege kuitambulisha video ya ngoma aliyofanya na Runtown, SA na Nigeria
Chege Chigunda amesafiri kuelekea nchini Afrika Kusini na baadaye ataelekea Nigeria ili kuweka mazingira mazuri ya kuanza kuitambulisha video ya wimbo aliomshirikisha Runtown wa Nigeria.
Meneja wa TMK Wanaume Family, Said Fella ameiambia Bongo5 kuwa video na wimbo huo kwa hapa nyumbani vitaachiwa December 4.
“Chege yupo South kwaajili ya ile kazi na Runtown,” amesema Fella.
“Hapa nyumbani itatambulishwa tarehe 4 lakini hivi karibuni Chege ataanza kuitambulisha South Africa na Nigeria.”