Burudani
Cassper Nyovest awa rapper wa kwanza SA kufikisha followers milioni 1 Instagram
Cassper Nyovest amekuwa rapper wa kwanza nchini Afrika Kusini kufikisha followers milioni 1 kwenye mtandao wa Instagram.
Rapper huyo wa Doc Shebeleza amefikisha idadi hiyo ya followers wiki hii.
Mpinzani wake, AKA bado anacheza kwenye 783k. Hata hivyo AKA anamkimbiza Cassper kwenye Twitter akiwa na followers milioni 1.2, karibu mara mbili ya alionao Cas.
Kwa Tanzania bado hakuna rapper mwenye followers milioni 1. Ni Joh Makini hata hivyo ndiye atakayeifikia soon. Hadi sasa ana followers 992k.