Burudani
Busta Rhymes aondoka kwenye label ya YMCMB
Busta Rhymes sio member wa YMCMB tena. Baada ya kukaa miaka miwili na label hiyo, rapper huyo mkongwe ameondoka Cash Money.
Akiongea kwenye kituo cha SiriusXM cha ‘Sway in the Morning’, Bussa Buss amedai kuwa kuondoka kwake ni kutokana na kutooelewana katika masuala ya kiubunifu.
Busta amesonga mbele na career yake na mapema mwezi huu aliachia single yake ‘Calm Down’ aliyomshirikisha Eminem na anaanda album yake ya 10, E.L.E. 2.