Burudani
Bruno Mars, Adele, John Legend na wengine kutumbuiza kwenye tuzo za Grammy mwaka huu
Waandaaji wa tuzo za Grammy wamemtangaza Bruno Mars kuwa miongoni mwa wasanii watakaotumbuiza katika utoaji wa tuzo hizo mwaka huu.
Bruno anaungana na wasanii wengine ambao wametangazwa kuwasha moto katika jukwaa hilo akiwemo Adele, John Legend, Metallica, Carrie Underwood na Keith Urban. Wakati huo huo hitmaker huyo wa 24K Magic amechaguliwa kuwania tuzo hizo kupitia kipengele cha ALBUM OF THE YEAR.
Tuzo hizo zinatarajiwa kufanyika Jumapili ya February 12, 2017 katika ukumbi wa Staples Center uliopo mjini Los Angeles.