Diamond PlatnumzWema Sepetu

#BringBackOurWema: Ujumbe wa Diamond umeonesha ni Wema ndiye anayehitaji kubadilika!

Tuseme na ule ukweli… Kila mmoja katika maisha ya uhusiano amewahi kuongea maneno kwa hasira kwa mpenzi wake na baadaye kuja kugundua kuwa yalikuwa makali kiasi cha kumuumiza mwenzi wake. Hii inatokea sana, na after all sisi wote ni binadamu na sijawahi kusikia kuna binadamu aliyewahi kuishi kwenye ulimwengu huu akatajwa kuwa alikuwa mkamilifu.

wema

Udhaifu ni miongoni mwa sifa zetu wanadamu. Udhaifu huo ndio ulimfanya Diamond aandike ujumbe ambao kwa wengi umeonekana kama ni msumari wa moto kwenye moyo laini wa mpenzi wake Wema Sepetu.

Kabla ya kuanza kujudge mimi ni nani hadi niwajudge wawili hawa, naomba nimnukuu Akon ambaye hivi karibuni aliwahi kutoa maoni yake kuhusiana na tetesi za kuvunjika kwa ndoa ya Jay Z na Beyonce. Akon alisema: Ukiwa mtu unayejulikana na una uhusiano, uhusiano wako nao unakuwa wa umma. Hivyo usipofunguka kwa umma, ni kawaida wao kuongea vitu wanavyohisi vinaendelea.”

Akon alimaanisha kuwa uhusiano wowote wa watu wanaojulikana hugeuka kuwa uhusiano unaongaliwa na kila mtu. Mkiwa mastaa hamuwezi kuwa na uhuru tena.

Hivyo kwa muda mrefu mashabiki wa Wema na Diamond wamekuwa wakihisi kuna jambo lisilo sawa katika uhusiano wao. Mashabiki wa Wema waliamua kuanzisha kampeni ya #BringBackOurWema baada ya kuhisi kuwa ni Diamond pekee anayenufaika na uhusiano huo, huku career na CV ya Wema ikiendelea kushuka.

Wengi wanaamini kuwa Diamond amekuwa akitumia nguvu ya Wema kujiimarisha zaidi yeye. Ni kawaida hata hivyo kuwa mastaa wawili wakubwa wanapoungana, huwaangunisha pia mashabiki wao kuwa kitu kimoja. Na kwakuwa wote wawili kwa fani zao wana fanbase kubwa, muunganiko wao umetengeneza super fanbase.

Siku chache zilizopita niliandika makala kuhusu kufanana kwa mienendo ya Kim Kardashian na Wema Sepetu na nikadai kuwa tofauti yao ni jinsi Wema anavyoushusha ustaa wake kwa kukatika jukwaani kama dancer wa Diamond, wakati anatakiwa ‘kubehave’ kama first lady wa mwanamuziki anayependwa zaidi Afrika Mashariki kwa sasa.

PICHA: DIAMOND NA WEMA NI KAMA KANYE WEST NA KIM KARDASHIAN LAKINI…

Hicho, na mengine ndicho kimekuwa chanzo cha kuanzishwa kwa kampeni ya #BringBackOurWema.

Kwakuwa lawama nyingi zimetupwa kwa Diamond kuwa ndiye chanzo cha kuporomoka kwa heshima ya Wema huku wengi wakidhani kuwa staa huyo wa muziki haonekani kutoa msaada wowote kwa mwandani wake, ilikuwa ni lazima Diamond ajibu kwanini hali iko hivyo.

Niliwahi pia kuandika makala ya kumshauri Diamond atumie connection zake kumtafutia mashavu ya kimataifa Wema Sepetu.

KWANINI WEMA SEPETU HATUMII UMAARUFU WA DIAMOND KUTAFUTA FURSA YA KUFANYA FILAMU ZA KIMATAIFA?

Hata hivyo inaonekana Diamond aliuzingatia ushauri huo kwakuwa mwezi June mwaka huu alidai kuanza kumuunganisha na waigizaji wa Ghana.

DIAMOND AMUUNGANISHA WEMA SEPETU KUFANYA FILAMU NA WAIGIZAJI WA GHANA

Kama alivyosema Akon kuhusiana na ukimya wa Jay Z na Beyonce kuhusiana na ndoa yao kiasi cha kuwafanya watu wawe na ‘speculations’ cha kile wachohisi kinaendelea, ndivyo hivyo ingekuwa kwa Diamond kama angeamua kutumia ukimya kama jibu la kampeni hiyo.

Bahati mbaya, majibu ya Diamond kupitia Instagram yamekuwa makali kiasi cha kuwashtua wengi na kuona kama kamkosea heshima mpenzi wake. Kwakuwa sitaki kuonekana kama namhukumu Diamond kwa kile alichoandika, ningependa kuongea kwa lugha ya busara kadri iwezekanavyo, na isitoshe nimegusia suala la ‘udhaifu’ na ‘ubinadamu’ katika aya zangu za mwanzo.

Diamond ametumia kauli nzito na ya hasira kidogo katika kuwajibu vinara wa kampeni hiyo. Si jambo la busara kumuita mtu umpendaye kwa kuandika ‘msanii wenu’ baada ya jina lake, pale alipoanza kwa kuandika: Nafikiri ningewaona kweli Mnaakili na Mapenzi ya dhati kwa ‘Msanii wenu’. Ingekuwa vyema kama angeandika; Nafikiri ningewaona kweli Mnaakili na Mapenzi ya dhati kwa ‘Wema Sepetu’. Again, hizo ni hasira tu na ndio maana aliamua kuifuta post hiyo.

Kwa maelezo aliyoyatoa staa huyo, imebainika wazi kuwa ni Wema ndiye aliyeamua kuishi hivyo na pengine ameridhika na hatua aliyofikia. Inavyoonekana Diamond hapendwezi na muenendo na maisha ya mpenzi wake hasa kwa kudai anaendekeza urafiki na watu wanaopenda anasa na kula bata.

“Mngemshauri apunguze mashoga wapenda anasa na apunguze starehe zisizo na faida, wenda ingemsaidia pesa kuzitumia kwenye kufanya kazi na kuleta maendeleo badala ya kuwapa viwanda vya pombe,” yanaendelea kusomeka majibu ya Diamond. Maelezo hayo yanaeleweka wazi kuwa Wema amekuwa ni mtu wa starehe na kula raha na marafiki zake (Aunty Ezekiel haikwepi hii sentensi, inamhusu). Kwa kauli ya Diamond, Wema anaonekana kuendekeza ulevi kwa kutumia fedha anayopewa na mchumba wake.

“Mimi kama bwana, wajibu wangu ni kuhakikisha mpenzi wangu anakula vizuri, anavaa vizuri, analala vizuri, na kumwezesha mtaji wa kufanyia kazi.”

Sentesi hiyo inamaanisha kuwa, Diamond anatimiza wajibu wake na tayari amempa mtaji mpenzi wake. Kuna taarifa pia kuwa hata filamu yake ya Family aliyoigiza na Aunty Ezekiel ilidhaminiwa na Diamond.

“Waswahili wanasema mchungaji bora anatakiwa kuhakikisha anampeleka ng’ombe wake kwenye maji safi, ila yeye ng’ombe mwenyewe ndio anatakiwa aamue kunywa maji,” anaendelea Diamond. “Au mnataka nikishampa mtaji niache kufanya na show tena na kuigiza nimuigizie mie ? Nisiende studio nikae dukani nimuuzie mie? Ni juhudi zako kwanza.”

Maneno ya Diamond yanajielezea yenyewe kuwa Wema amejisahau. Maswali ya wengi ni kuwa wao kama wapenzi hawajawahi kuzungumza haya na kushauriana? Diamond hajawahi kumkanya mpenzi wake kuwa mwenendo wake sio? Au ameshamuambia hadi amechoka na ndio maana ameamua kuuambia umma kile kinachoendelea?

Kwa lawama na matusi ambayo Diamond ameyapata kutokana na kampeni hiyo, ilikuwa inahitaji uvumilivu wa hali ya juu kukaa kimya. Nahisi uvumilivu ulimshinda na ndio maana aliamua kuandika alichokiandika ambacho bahati mbaya kinaweza kutia tena doa uhusiano wao. Sijui Wema atasemaje!!

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents