Habari
Breaking: Lema ashinda rufaa yake, sasa kuwa mbunge wa Arusha tena
Hatimaye aliyekuwa mbunge wa Arusha Godbless Lema amekuwa tena mbunge wa Arusha baada ya kushinda katika rufaa ya kesi yake ya kupinga matokeo.
Rufaa hiyo imesomwa leo jijini Dar es Salaam.
Lema alivuliwa ubunge Aprili 5, 2012 katika hukumu iliyotolewa na Jaji Gabriel Rwakibalira, kutokana na kesi iliyofunguliwa na makada watatu wa CCM; Mussa Mkanga, Happy Kivuyo na Agnes Mollel, wakipinga ushindi wake katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.