Breaking: Kariakoo pachafuka, mabomu yanapigwa kila kona
Habari zilizotufikia hivi punde zinadai kuwa kuna hali mbaya katika maeneo ya Kariakoo jijini Dar e Salaam ambapo polisi wanapiga mabomu ya machozi kutawanya waislam wanaoandamana.
Kwa mujibu wa watu waliopo kwenye maeneo hayo maduka mengi yanafungwa na watu wanajifungia kwenye maduka hayo.
“Nipo maeneo ya kurasini, kuna helkopta ya polisi imepita katika anga hili muda huu. Sijui inaelekea wapi?” anasema shuhuda mmoja.
Naye mtangazaji wa Channel Ten, Salma Msangi ameandika kupitia Twitter, “Tanzania ya leo kama IRaQ, napita barabarani napishana na ma defender tu na mitutu, ndo twalindwa au wanalindaaa. Tanzania imeharibika tobaaaa, Waislam vs police.”
“Maandamano yameanza huku Mwananyamala….. Sauti za bunduki zinasikika!”
Tutaendelea kukupa updates kadri inavyowezekana.