Bow Wow kutua Bongo?!
Inasemekana kwamba mwezi ujao msanii maarufu wa Hip Hop, Bow Wow atatia mguu Afrika ya Mashariki kwa show kadhaa. Maneno mitaani zinasema promota kutoka Uganda Hemdee Kiwanuka yupo katika harakati za kutafuta sponsor kwa ajili ya onesho la Nairobi, wakati maonesho yameshapangwa jijini Dar es Salaam na Rock City aka Mwanza.
Kama ni kweli, Bow Wow anaetamba na vibao vyake kama “You Can Get It
All”, “Big Girls” na “Roc The Mic” atakuwa msanii wa kwanza wa
kimataifa kutua nchini kwa mwaka huu wa 2009!