Burudani
Born2Shine Clothing Line ya B12 yapata mwekezaji mkubwa
Mtangazaji wa redio na mjasiriamali wa fashion, Hamis Mandi aka B12 amesema amepata wawekezaji ambao wataifanya brand yake ya Born2shine Clothing Line na maduka yake kuwa kubwa zaidi.
Akizungumza katika kipindi cha Mkasi, mtangazaji huyo wa Clouds FM alisema katika siku za baadaye kampuni yake itakuwa kubwa zaidi.
“Mimi nimejipanga, nimeinvest,” alisema. “Nina duka langu la nguo Bonr2Shine ambalo linafanya vizuri na in the near future Born2Shine tayari imepata mwekezaji. Kwahiyo ni kitu kingine kikubwa kitakuja baadaye.”