Michezo

Boniface Mkwasa aahirisha kambi ya Taifa Stars

Kutokana na maombi ya klabu nyingi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kutaka kuandaa wachezaji kwa ajili ya Ligi Kuu msimu unaoanza sasa, umemlazimu Kocha Mkuu timu ya Mpira Tanzania ‘Taifa Stars’, Charles Boniface Mkwasa kuahirisha kambi iliyokuwa ianze Jumatatu Agosti mosi, mwaka huu, imefahamika.

mkwasaserena

Wachezaji ambao Mkwasa amewaita wanatoka kwenye klabu mbalimbali na ambazo zinaongoza kutoa nyota wengi ni Simba SC, Young Africans SC, Azam FC na Mtibwa Sugar FC.

Hivyo basi, Mkwasa sasa atakuwa anafuatilia mwenendo wa nyota 24 aliowaita kwenye michezo mbalimbali ya kirafiki wa klabu hizo inayofanyika kabla ya kuanza Ligi Kuu Tanzania Bara (Pre-season matches) na michezo ya raundi ya kwanza na pili ya Ligi Kuu kabla ya kukiita tena kikosi hicho kwa ajili ya safari ya kwenda Nigeria.

Taifa Stars ina mchezo na jijini Lagos, Nigeria Septemba 2, 2016 ambao ni wa kukamilisha ratiba katika kundi G baada ya Misri kusonga mbele wakati Chad kujitoa. Wachezaji ambao Mkwasa aliwaita mapema wiki hii ni:

Makipa:

Deogratius Munishi

Aishi Manula

Benny Kakolanya

Mebeki:

Kelvin Yondani

Aggrey Morris

Oscar Joshua

Mohamed Husein ‘Tshabalala’

Juma Abdul

Erasto Nyoni

Viungo:

Himid Mao

Mohamed Ibrahim

Shiza Kichuya

Jonas Mkude

Ibrahim Jeba

Mwinyi Kazimoto

Farid Mussa

Juma Mahadhi

Hassan Kabunda

Washambuliaji:

Simon Msuva

Joseph Mahundi

Jamal Mnyate

Ibrahim Ajib

John Bocco

Jeremia Juma

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents