Burudani
Bongo5 SWAGG ya Miaka 50 ya Tz
Kampuni ya Bongo5 inapenda kuungana na Watanzania wote katika kusherekea miaka 50 ya Uhuru wa Amani katika nchi yetu kwani ni jambo pekee la kusifiwa na kufanya nchi yetu iendelee kutambulika kama kisiwa cha Amani duniani.
Pia Bongo5 inawatakia viongozi na watanzania wote moyo wa kuwa na subira, uvumilivu, upendo na uzalendo kwa nchi yao katika kuendelea kuitunza Amani ili kuweza kutimiza miaka 50 mingine tutakayoianza hivi karibuni.
Kama Bongo5 tutaendelea kukuletea burudani zote, ambazo tumekuwa tukitoa siku zote, kuanzia New Audio, New Video, Interview, na stori motomoto, ambazo zimekuwa chachu ya stori zingine kuibuka.
Endelea kufuatilia kila siku hapa Bongo5…
Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki BONGO5