Bongo Movies: Majuto, Hemedy, Johari watoa filamu mpya (Picha)
Hemedy, Mzee Majuto na Johari wameingiza sokoni filamu zao mpya.
Nao Mzee Majuto na Hemedy wameachia filamu yao Kimbulu iliyofanyika jijini Mwanza.
“Sio kila unayemkuta kijijini ni mshamba wengine wanajua na wanaweza kuliko wewe. Mzee Mbunda na wajukuu zake jembe na edo madirector kutoka mjini wanaingia kijijini na kuwa na maisha ya KIMBULU. yaan paka lililoshindikana ila wanakwaa visiki baada ya kukutana na wanakijiji wanaojua zaidi yao,” yanasomeka maelezo ya filamu hiyo.
Filamu nyingine iliyoingia sokoni ni Wrong Hope iliyochezwa na Blandina Chagula maarufu kama Johari.
“Siwezi kuwa mimi bila nyinyi wrong hope hope ni movie mpya kutoka rj company na ni movie ya mwisho aliyoshiriki kipenzi chetu ambaye hatuko naye tena Recho Saguda,” ameandika Johari.