Bonanza leo laingia siku ya pili
Katika kuendelea kwa burudani pale kwenye viwanja vya Leaders Club, mambo yalikuwa babu kubwa kwa siku ya jana pindi walipopanda wasaniii mbalimbali, wakiwemo Tip Top Connection, Diamond, Linex na wengine wengi. nazidi kukusisistizia bado
haujachelewa, elfu saba yako mkononi wahi ukajipatie burudani ikiwemo nyama choma, mchezo wa Golf, Pool table na kila aina ya mchezo wewe unaopenda.
Kuna kila aina ya bia… kali na zile za watu kama sisi… zipo bia mpaka unaweza kusema ni Perfurm zinavyopendeza
Nani asiyeweza kucheza kwaito….kama unajijua huwezi.. sogea Leaders Club sasa hivi, uone kazi inavyofanyika… kwaito inaraha yake unapocheza kwa mtindo tofauti…
Godzilla naye alikuwepo, na mwanamuziki Diamond wote waliweza kufanya mambo makubwa.
Sio wakubwa peke yao hata watoto tumewajali, hivyo walete watoto wako iliupongoze kero za kukudai sehemu ya kwenda wikiend hii
Kila kitu kinachofanyika kwenye mwili wa mwadamu na kukifurahia basi hiyo pia ni burudani, na ndivyo ilikuwa na inaendelea pale kwenye viwanja vya Leaders Club kwa kukupa kile ukipoendacho, kuhusiana na kile ukipendacho hata kama unapenda urembo kama hivii…