Blogger mtata wa Kenya ashtakiwa kwa kumuita Kenyatta ‘Rais Mtoto’
Blogger maarufu wa Kenya mwenye ushawishi mkubwa kwenye Twitter, Robert Alai ameshtakiwa kwa kumdhihaki Rais Uhuru Kenyatta kwa tweet aliyoandika mapema wiki hii.
Alai ambaye ni mkosoaji mkubwa wa serikali, alimuita Kenyatta ‘Rais Mtoto’.
Amekanusha madai hayo na alitolewa kwa dhamana ya $2,000 na kuonywa kutoandika tweets za aina hiyo wakati uchunguzi ukiendelea.
Meanwhile in Machakos @DrAlfredMutua is trying to pull Jubilee's @RobertAlai stunt on @Ken_Wamaria and Co. Wueh!! pic.twitter.com/iembVKyREz
— Akamba Warrior (@Mwolooto) December 18, 2014
Alai ana followers zaidi ya 141,000 kwenye Twitter. Siku hiyo hiyo alipoandika tweet hiyo, alipost pia namba ya Kenyatta na za maafisa wengine wa juu.
Wakenya wengi wanaoamini mashtaka hayo ni sehemu ya mpango wa serikali kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari na wa kujieleza, wamemuunga mkono kwa Alai.