Burudani
Black Coffee akamilisha collabo yake na Alicia Keys
Mshindi wa tuzo ya BET kwenye kipengele cha Best International Act: Africa, Black Coffee amekamilisha kufanya collabo yake na Alicia Keys.
Akiongea na Sunday Times, Black Coffee amekubali taarifa hizo kuwa za kweli lakini alikataa kuweka kila kitu wazi kwa kusema, “can’t keep telling people everything I’m doing, as it may bore people.”
Jina la Black Coffee limeonekana kuwa geni kwenye masikio ya wengi lakini huyu ni mmoja kati ya wasanii wenye heshima kubwa Afrika Kusini na mpaka sasa amefanikiwa kuachia albamu sita na tayari ameshakutana na mastaa wakubwa akiwemo Diddy na Wiz Khalifa alipohudhuria tamasha la Ultra Music [Festival] lililofanyika, March 2016, Miami.