Burudani

Billnas adai wimbo wake mpya ‘Mazoea’ aliurekodi miaka 3 iliyopita

Msanii wa muziki wa hip hop, Billnas amedai wimbo wake mpya ‘Mazoea’ aliyomshirikisha rapper Mwana FA aliurekodi toka mwaka 2014.

Rapper huyo ambaye yupo chini la label ya LFLG, amedai amekuwa na tabia ya kurekodi nyimbo nyingi na kuziweka kusubiria muda sahihi wa kuziachia.

“Nyimbo ya mazoea nilirekodi tangu mwaka 2014,” Billnas alikimbia kipindi cha Ubaoni cha EFM. “Unajua ukiwa na nyimbo nyingi ndani kuna utulivu fulani unakuja kwa msanii, kwa sababu tayari ndani una ngoma za kutosha ambazo zinasubiria muda wakutoka,”

Kuhusu wimbo wake wa ‘Mazoea’ rapper huyo amedai ameachia wimbo huo ili kuwataka watu kupunguza mazoea kwani mazoea hupunguza heshima.

“Mtu hawezi kutunza heshima kama akikuzoea sana,” alisema Billnass.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents