Burudani
Ben Pol: Msanii kujisimamia mwenyewe inaua ubunifu
Ben Pol anaamini kuwa pindi msanii anapojisimamia mwenyewe, anapoteza ubunifu muhimu anaouhitaji ili kufanikiwa.
Anadai kuwa ni muhimu kwa msanii kuwa na management au watu wa kumsaidia.
“Ni muhimu kwasababu kwanza ukifanya vitu vingi kwa msanii inachosha, inaua ule upande wa creativity kwenye utunzi labda, kujifikiria namna ya kujiboresha wewe kama msanii, sauti na vitu vingine,” Ben Pol alikiambia kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz cha EATV kwenye mahojiano ambayo hayakuruka kwenye TV (Extended).
“Inakula sana time, we uanze kupigia simu director, promota, yaani inakata sana, kwahiyo ni vizuri kuwa na either manager au timu ambao wanakuelewa unachotaka,” aliongeza.