Burudani

Ben Pol aahidi surprise ya video 2013 mwanzoni

Hit-maker wa Pete, Ben Pol amesema ataufungua mwaka 2013 kwa video mpya itakayokuwa surprise.

Akiongea na Bongo5 Ben Pol amesema, “inaweza ikawa ni kitu ambacho watu hawakutegemea na inaweza ikawa kitu ambacho watu watashtuka lakini watapenda.”

“Kwanza kabisa mimi video yangu iliyopita sikuonekana sana ambayo ni ya “Maneno maneno” ni video ambayo mimi sijacheza wamecheza watoto wale kwahiyo video inayokuja watu wanataka kujua na mimi mwenyewe nitakachokifanya nikumpeleka Ben pol mpya kimwenekano na kwa kila kitu na hiyo ni kwasababu Ben Pol wanahitaji kumuona hajaonekana kwa muda mrefu kwahiyo wamemmiss sana.”

Ben Pol amesema video itafanyika hapa hapa nchini Tanzania na gharama ambayo ataitumia takriban milioni 6. “Sasa hivi siwezi kufanya video chini ya bajeti ya milioni 3 au 4 kwa sababu mimi mwenyewe najiogopa naona music unaweza kunilipia nikafanya video mzuri,” amesema Ben.

“Kwa swala la production bado tupo kwenye mazungumzo sijajua nipo wakati wa mwisho na uongozi wangu kujua itafanyikia studio gani lakini mpaka mapema mwakani nitatoa taarifa kwasababu sasa hivi tupo kwenye mazungumzo ya mwisho.

“Video yangu itakuwa ni surprise ndiyo maana sijasema itakuwa ya wimbo gani watu kitu ambacho watategemea kinaweza kisiwe lakini mwisho wa siku wataenjoy sitaki kuwa dissapoint mashabiki wangu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents