Technology
Beats Music kuwekwa kwenye Iphone na Ipad zote kuanzia mwakani
Kampuni ya Apple imedai kuwa app ya Beats Music itakuwa sehemu ya software ya iOS kuanzia mapema mwakani na itapatikana kwenye iPhone na iPad zote.
Financial Times limedai kuwa Beats itakuwa sehemu ya iOS mapema March ikiwa ni jitihada za Apple kuwafanya watumiaji wa iTunes kuijaribu huduma hiyo ya kustream nyimbo watakaoweza pia kulipa kupitia huduma ya Apple Pay kwaajili ya malipo ya kila mwezi ya huduma hiyo.
Apple iliwalipa dola bilioni 3 kampuni baba ya Beats Music, Beats Electronics ya Dr Dre mapema mwaka huu. Beats Music inatarajiwa kuwa mshindani mkuu wa huduma zingine za aina hiyo hasa Spotify na Rhapsody.