Burudani
BBA: Laveda na Permithias wabusiana kama wamebakiza siku moja ya kuishi (Picha)
Hakuna siri kuwa siku za kuendelea kuwepo kwa mwakilishi wa Tanzania, Laveda kwenye shindano la Big Brother Africa Hotshots zinahesabika.
Baada ya kukwepa eviction wiki iliyopita, wiki hii alirejea tena kikaangoni na huenda mashabiki wa shindano hilo wameanza kuchoka kelele zake za saxophone kwakuwa wamekuwa wakimtaja zaidi kuwa wangependa kuona anafungasha virago.
Hata hivyo hilo halimpotezei haki yake ya kufurahia maisha ya mjengoni na fursa ya kupata mtu wa kumliwaza. Bahati hiyo imemwangukia Permithias ambaye alijikuta akibadilishana mate na Laveda kama vile wamebakiza siku moja ya kuishi.