Michezo
Bastian Schweinsteiger ajiunga ligi kuu ya Marekani
Kiungo wa klabu ya Manchester United Bastian Schweinsteiger amejiunga na klabu ya Chicago Fire inayoshiriki ligi kuu ya Marekani MLS, kwa mkataba wa mwaka mmoja wenye thamani ya dola milion 4.5
Nahodha huyo wa zamani wa timu ya Ujerumani ameruhusiwa kuondoka na klabu ya Manchester United kufuatia kutokuwepo kwenye mipango ya kocha Jose Mourinho.
Anataraji kujuinga rasmi na timu hiyo wiki ijayo baada ya kukamilisha masuala ya Visa na vipimo vya afa
Schweinsteiger mwenye miaka 32, amejiunga na Manchester United Julai 2015 akitokea katika klabu ya Bayern Munich