Banana Zorro aingia darasani kujifunza muziki wa Hip Hop, mwalimu ni Mwana FA
Banana Zorro anataka kuongeza kitu kipya kwenye muziki wake. Muimbaji huyo ameingia darasani kujifunza muziki wa hip hop na mwalimu wake ni Hamis Mwinjuma aka Mwana FA.
Banana amekiambia kipindi cha XXL, cha Clouds FM kuwa tayari ameshaanza darasa hilo.
“Mimi naimba muziki wote lakini FA ananI-train Hip Hop,” amesema. “Moja sio kwamba nafanya ndo nitakachofanya. Experience watu soko linabadilika, limekua. Hata kurekodi bado hata hata training bado sijamaliza. Nauliza maswali na yeye ananipa style. Hakuna muziki unaouza zaidi ya muziki mwingine ila kinachotokea nyimbo nzuri yoyote inaweza kuuza zaidi ya nyimbo nyingine yoyote. Lakini pia imetengenezwa vizuri. Kikubwa ni kuwa creative kutokana na soko ndio linavyotaka na soko lipo tayari kwa kazi yoyote nzuri.”