Habari
Bamboo: Mungu aliniambia ‘sikukuita Bamboo’, aelezea sababu za kubadili jina na kuwa Abraham
Rapper mkongwe wa Kenya Simon Kimani a.k.a Bamboo ambaye kwa sasa ameokoka, hivi karibuni ametangaza kubadili jina lake kutoka Bamboo ambalo amekuwa akilitumia katika muziki wa kidunia na sasa anataka aitwe Abraham (Ibrahim).
Rapper huyo tayari amebadili jina lake katika akaunti yake ya facebook na kuwa Abraham Bamboo, na kuelezea sababu za yeye kubadili jina:
“Mungu aliniambia kitu, alisema ‘sikukuita “Bamboo” dunia ndiyo ilikuita hivyo lakini mimi nilikuita kama nilivyokuumba na jina lako ni “Abraham”. Abraham Bamboo linaweza kuwa jina lako kisanii . “ aliandika Bamboo katika akaunti yake ya Facebook.
Abraham Bamboo ni kaka wa mastaa wengine wa Kenya Victoria Kimani pamoja na ambao wote ni wasanii wa muziki