Burudani

Baby Madaha kuachia wimbo mpya ‘Mahaba Niue’

Msanii wa filamu na muziki, Baby Madaha amezungumzia ujio wa kazi zake mpya za muziki na filamu ambapo amesema hivi karibuni ataachia wimbo wake mpya uitwao ‘Mahaba Niue.’
Baby Madaha akifuatilia mdahalo

Baby ambaye yupo Dar es Salaam kwa sasa ameiambia Bongo5 kuwa amepokea maoni mengi kutoka kwa mashabiki kuhusu nyimbo za mapenzi.

“Kuna two song, kuna moja inaitwa Mahaba Niue ambayo nimeimba mapenzi , mashabiki wangu wameniambia wamenimiss katika mapenzi, nimerudi kidogo kwenye mapenzi. Producer anaitwa Hash na studio inaitwa Motherland ni producer mpya ametoka Finland. Kwahiyo nikamcheki nikaona ninaweza kufanya naye kazi,” amesema Baby Madaha.

Pia amewataka mashabiki wake kusubiria filamu mpya pamoja na ujio wa tamasha kubwa la muziki litakalofanyika Tanzania baada ya kufanyika huko nchini Kenya.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents