Burudani
Baba yake Paul Walker naye awashtaki Porsche kwa kifo cha mwanae
Baba yake na Paul Walker Jumatano hii amewasilisha mashtaka dhidi ya kampuni ya magari ya Porsche akidai kuwa gari ambalo mwanae alikuwa akiendesha lilikosa vitu vya kiusalama ambavyo vingeweza kuokoa maisha yake.
Muigizaji huyo wa Fast & Furious alifariki November 2013 kwenye ajali mbaya ya gari huko Santa Clarita, Calif., iliyomuua pia rafiki yake Roger Rodas, dereva wa gari aina ya 2005 Porsche Carrera GT.
Mashtaka hayo ni kama yale yaliyowasilishwa na mtoto wa Meadow, September.
Awali Porsche ilidai kuwa ni Rodas ndiye aliyekuwa na makosa hadi kutokea kwa ajali hiyo.