Burudani
Baada ya Vee Money na Joh Makini, sasa ni zamu ya Shaa kwenye Coke Studio Africa
Mwaka huu Coke Studio Africa imeamua kuchukua wasanii wengi zaidi nchini kushiriki kwenye kipindi hicho.
Shaa akiwa na Jackie
Baada ya Vanessa Mdee kuungana na msanii wa Nigeria, Burna Boy na Joh Makini kurekodi na Chidinma wa Nigeria, sasa ni zamu ya Shaa ambaye yupo Nairobi, Kenya kurekodi kwenye kipindi hicho na msanii wa Uganda, Jackie Chandiru.
“Ndani ya #CokeStudioAfrica wiki hii Malkia wa Uswazi nikiwa na @JackieChandiru #WanawakeOyeeee hahahah,” ameandika Shaa kwenye Twitter.