Habari
Baada ya UK, Ommy Dimpoz kufanya show Muscat, Oman mwezi ujao
Mwimbaji wa hit song ‘Tupogo’ Ommy Dimpoz ambaye kwa sasa yuko kwa Malkia Elizabeth Uingereza, baada ya kufanya show katika siku ya Valentine jijini London, sasa anatarajia kufanya show yake ya mwisho nchini humo mwezi March mwaka huu kabla ya kuelekea Oman.
Ommy aka mr PKP amesema show yake ya mwisho ya UK katika ziara hiyo sasa itafanyika March 1 katika mji wa Northampton na baada ya hapo ataelekea Muscat mji mkuu wa Oman kwaajili ya show nyingine.
“Lets Do this Again…..My Last show in UK kabla sijaelekea MUSCAT OMAN wajanja wote 1st of March tunakula bata na PozkwaPoz ndani ya NORTHAMPTON UK HATAREEEEeeeeeeee!!!!!!!” Aliandika kupitia Instagram.