Burudani
Baada ya misiba mitatu mfululizo, Amini kurudi na wimbo mpya, ‘Mbeleko’
Baada ya kupata misiba kwa kufiwa na kaka zake wawili na dada yake (wote wa tumbi moja), Muimbaji na mtunzi wa nyimbo kutoka THT, Amini Mwinyimkuu anatarajia kurejea tena kwenye muziki.
Amini amesema misiba hiyo ameichukulia kama mitihani katika maisha na ni kazi ya Mungu na kwamba ataachia wimbo mpya uitwao ‘Mbeleko’.
“Huu ni wimbo tofauti na watu walivyonizoea,” ameiambia Bongo5.
“Ni wimbo wa asili yetu Tanzania, na nimeimba mambo ya jamii kwa watu kupendana zaidi. Na sasa hivi nipo location nashoot video. Nashoot na HK Production, kwahiyo mashabiki wangu wasubiri kazi yangu mpya.”