Burudani

Baada ya kusikika tena kwenye XXL, DJ Fetty ajibu kama amerejea rasmi Clouds

Ijumaa ya November 20 ilikuwa ni siku ya furaha kwa wasikilizaji wengi wa Clouds Fm hasa wa kipindi cha burudani XXL, baada ya kupata surprise ya kumsikia tena mtangazaji maarufu na anayependwa Fatma Hassan maarufu kama DJ Fetty kwenye kipindi hicho, ikiwa ni miezi miwili imepita toka alipotangaza kuacha kazi ya utangazaji September 15 mwaka huu.

Fetty2

Wengi wao walicomment kwenye akaunti zake za mitandao ya kijamii kuelezea furaha yao, na kwasababu hakusema kama amerudi rasmi kutangaza au laa, wengine waliamini kuwa mtangazaji wao amerudi.

Bongo5 ilimtafuta Fetty kutaka kufahamu kama ni kweli amerudi Clouds na ataendelea na kazi ya utangazaji, na jibu lake lilikuwa “Sijarudi”..

Fetty-2

Na kuhusu sababu ya kusikika kwenye XXL ya Ijumaa November 20 alijibu;

“Baada ya kuona kwenye acc ya insta yangu, they want to hear me so badly so nika wa surprise tu hivyo. But Sipo clouds” alisema Fetty.

Hizi ni comments za mashabiki wake baadaa ya kumsikia jana;

tamimugau- Hatimae umesikka katka kipind cha XXL…..tujuze labda kwnn uliamua kuacha kaz zen leo umerudi????

issathebwse- Jaman dada mbona umepotea kesho nenda studio tukuskie hata sauti jaman mie roho inaniuma sana

jumawaukwel- Fetty nimeijoi xana xxl leo ujue nilikua xhamba nafanya yangu nikapigiwa cm na mwanagu kwamba fee yupo mjengoni leo nikaacha kufanya yangu kuja kukusikiliza ww

elbasharsaid- UMERUDI or ulikuja kutuonjesha ladha tu alafu ndo jii tena Ama kweli kama umerudi big up Sana my @the best de

mamyakaro- Utuambie kama umerudi rasmi fetty coz nilizira kabisa kuckiliza xxl ila leo nilipockia tu sauti yako kwa mjengo bac daaaah,nikaahirisha kabisa kwenda kuoga@thebestfetty

candlesuleiman- Am back 2! Love u forever @thebestfetty. Ahsante kw kurudisha mood zetu uloamua kukimbia nazo name sasa umerudi nazo. Hapo surprise tu!

mwajabus92- Nimefurahi sana nilivyosikia sauti yako Leo clouz yani nilikuwa nakumiss hatari ndio umerudi moja kwa moja au ndio Leo ulikuja kutufurahisha love yo feeeee

zephaniamagesa82- umerudi nini yani toka uwondeke sijawahi sikiliza nijibu kama umerudi jamani my dj

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents